Lyrics : Stamina Ft Barnaba – Safina

Stamina Ft Barnaba - Safina
Stamina Ft Barnaba – Safina

Lyrics : Stamina Ft Barnaba – Safina

Download : Stamina Ft Barnaba – Safina

Halleluyah, Halleluyah
Halleluyah, Halleluyah
Halleluyah, Halleluyah
Halleluyah, Halleluyah

Baba kabla haujashusha gharika kwa nchi nzima
Umenituma dumu mwanao nije nijenge safina
Napo sema Mungu ni mkubwa, ni ukweli sio poyoyo
Amemfanya hadi kiziwi anaskia mapigo ya moyo

Dini sku hizi zinavuma kwa upepo wa kisulisuli
Sioni ibada wanashindana kuvaa vizuri
Safina haina nafasi kwa watumishi mabishoni
Ndio maana siingizi wachungaji maana watakula kondoo

Umenipa madada mnnajishoot uchi sio poa
Umenipa makaka mbaya wengine makaka poa
Mwanamke kuwa mwanaume wa mwanamke asiye na mume
Ni mwanaume tena wa kiume kuwa mwanamke wa mwanaume

Shuleni hawafundishwi somo linaloitwa utajiri
Bali dhamani ya x ambayo mtaani haiwapi dili
Wacha watoto waje kwako ila kwa mwendo wa polepole
Wakumbuke tu, mkono wa sweta haunaga vidole

Lalala..

Kikubwa naomba Mungu
Aninusuru na maisha yamezidi kunichanganya
We tazama dunia
Wanakondoo na waumini kwenye safina ndo wanazama

Oooh Jah Jah bless
Jah Jah bless
Oooh Jah Jah bless
Yes sir!

Kwenye mapenzi wanaenzi ilimradi
Ukiitwa mpenzi bila pesa we ni mpenzi mtazamaji
Unaeza ukafa leo, wanawe wakalia usiku na mchana
Ila cha ajabu mkeo, siku ya matanga kapata bwana

Ila Baba, samahani naomba nikuulize
Najua una mambo mengi na kimtindo uko bize
Ulisema tuzaliane ili tujaze dunia
Sasa ugumba na utasa uliweka wa nini?

Nafikiria anakamata bodaboda hajavaa helmet why?
Wakati kwa michepuko havai kinga anapiga dry
Pesa sio sabuni ya roho ni sabuni ya uchafu
Ingekuwa sabuni ya roho ingetakatisha mpaka wafu

Halafu Baba maisha ni mazoezi –
Ukiona watu wanakonda ujue pesa ndo gym tosha
Malipo ni hapa hapa duniani huko mbinguni hakuna change
Usihofu safina ikijaa wengine nitawalaza kweny kere

Lalala..

Kikubwa naomba Mungu
Aninusuru na maisha yamezidi kunichanganya
We tazama dunia
Wanakondoo na waumini kwenye safina ndo wanazama

Oooh Jah Jah bless
Jah Jah bless
Oooh Jah Jah bless
Yes sir!

Ndoto zilikuwa pilot, piloti
(Dreams come true, dreams come true)
Zilifeli baada ya kulost
(Dreams come true, dreams come true)

Ushabebeshwa mikoba ya kiganga
Ushavunja nazi njia panda
Ushale mgongoni wakakuchanja
Lakini bado hauna doh, doh doh doh…

Kikubwa naomba Mungu
Aninusuru na maisha yamezidi kunichanganya
We tazama dunia
Wanakondoo na waumini kwenye safina ndo wanazama

Oooh Jah Jah bless
Jah Jah bless
Oooh Jah Jah bless
Yes sir!

Halleluyah, Halleluyah
Halleluyah, Halleluyah
Halleluyah, Halleluyah
Halleluyah, Halleluyah

Stonebwoy Ft Kuami Eugene x Kidi – Take Me Away

Jamie

Call the classic man on +233542793417

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Back to top button